Habari Za Un

04 APRILI 2024

Informações:

Synopsis

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia ujumuishwaji wa wanawake katika masuala ya kifedha kwa lengo la kutimiza lengo la Umoja wa Mataifa la usawa wa kijinsia katika Nyanja zote. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na katika kujifunza kiswahili tunakuletea ufafanuzi na tofauti ya maneno “Adhuhuri na Alasiri”.Leo ni siku ya kimataifa ya uelimishaji kuhusu mabomu ya kutegwa ardhini na msaada wa kuchukua hatua dhidi ya mabomu hayo. Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, mabomu, vilipuzi na vifaa vingine vya mlipuko vinaendelea kuua na kujeruhi watu katika maeneo mengi yenye changamoto kubwa za migogoro duniani na matokeo yake vifaa hivyo vya mlipuko, kwa wastani hukatili maisha ya mtu mmoja kila saa, na waathirika wakubwa wakiwa ni watoto.Mratibu wa Misaada ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa katika eneo la Palestina linalokaliwa kwa mabavu, Jamie McGoldrick anaelekea Gaza leo. Umoja wa Mataifa unaeleza  kuwa mapigano makali kati ya wanajeshi wa Israel na makundi yenye silaha ya Palestina yanaendelea kur